LITURJIA NI NINI? NA JE IPO KIMAANDIKO?.

 


LITURJIA NI NINI? NA JE IPO KIMAANDIKO?.

Liturjia/Litrujia ni mwongozo wa jinsi ya kufanya ibada unaotumiwa na makanisa mengi.

Ibada inaundwa na vitu vikuu vitano, ambavyo ni Maombi, Neno, Matoleo, Sifa, na Meza ya Bwana. Vitu hivi vitano ndivyo vinavyoiunda ibada.

Kwahiyo ukiwapo mwongozo wowote wa jinsi ya kuviendesha vitu hivi, na mwongozo huo ukawekwa kwenye kitabu maalumu..Mwongozo huo ndio unaojulikana na wengi kama Liturjia.

Kikawaida hakuna kanisa lisilo na mwongozo, na ni jambo la kimaandiko makanisa yawe na mwongizo fulani, ili mambo yote yafanyike kwa uzuri na utaratibu..

1 Wakorintho 14:40 “Lakini mambo yote na yatendeke kwa uzuri na kwa utaratibu”.

No comments

Post a Comment

Shajara Yetu © all rights reserved
MKATOIKI KIGANJANI by mitume technologies