HISTORIA YA MT. PADRE PIO WA PIETRELCINA 23 SEPTEMBA




Historia ya Mt. Padre Pio wa Pietrelcina






Mtakatifu Padre alikuwa ni mmoja kati ya watoto 8 wa baba Forgione na mama Maria, ambapo watatu kati yao walifariki wakiwa bado wadogo. Wazazi hawa walikuwa wakulima wadogodogo.

Mt. Padre Pio alizaliwa tarehe 25.05.1887 kusini mwa Italia katika mji wa Pietrelcina. Alipewa jina la Fransisko kwa heshima ya Mt. Fransisko wa Assizi. Familia yao haikuwa tajiri, lakini waliishi maisha yaliyojawa na utajiri wa mapendo na amani. Hawakuwa na vitu vya ziada, ingawa mama yao alijitahidi kuwahudumia na kuwatunza watoto vizuri.

Kwa moyo wake wa ukarimu, mama Maria alipenda daima kwenda kuchukua matunda shambani na kuyagawa kwa familia maskini. Jambo hili lilichangia sana kukuza fadhila ndani ya Fransisko Forgione. Familia hii kweli ilikuwa nyumba ya sala, kwasababu pamoja na mambo mengine, walizoea kusali pamoja sala ya Rozari Takatifu kila siku usiku kabla ya kulala.
Tangu utoto wake, Fransisko alionekana kuwa amejaliwa neema ya kuwa na vipaji vingi vya pekee na alikubalika kwa Imani yake thabiti, na moyo wa mapendo na bidii katika sala. Alijaliwa neema ya kuwaona Yesu Kristo na Mama Bikira Maria pamoja na Malaika wake mlinzi.

Alipokuwa na umri wa miaka 10, Fransisko alipata hamu ya kujiunga na Shirika la Ndugu Wadogo Wafransisko Wakapuchini. Mwaka huo huo alisikia mahubiri mazuri sana yaliyomfanya atambue uzito wa wito wake wa kuwa mtawa.

Kwa bahati nzuri, wakati huo akiwa bado na mvuto wa kuishi maisha ya kitawa, alitokea Ndugu mmoja jina lake Campillo (Mkapuchini) aliyetembelea huko Pietrelcina. Campillo aliishi vizuri sana fadhila za unyenyekevu na udogo. Mambo haya yalizidi kuamsha zaidi hamu ya Fransisko, hata akaamua kuwataarifu wazazi wake juu ya nia yake njema. Mara baada ya taarifa hiyo, wazazi wake walifanya kila namna inayowezekana ili kumsaidia mtoto wao atambue vema wito wake.
Mwaka 1903, alijiunga na shirika la Ndugu wadogo Wafransisko Wakapuchini huko Morcone na akachukua jina la Ndugu Pio kwa heshima ya Papa Pius wa v, aliyekuwa mtakatifu msimamizi wa mji wa Pietrelcina.

Alifunga nadhiri za kitawa mwaka 1907 na akapewa Daraja Takatifu la Upadre mwaka 1910. Daima Padre Pio alionekana akiwa katika hali ya unyenyekevu, tafakari, utulivu na mwenye moyo wa sala.
Upendo wake kwa Yesu wa Ekaristi, ulikuwa kama moto uwakao. Alizoea kusema “Ni rahisi dunia kuwapo bila jua kuliko kuwa bila Misa takatifu”. Alikuwa na upendo wa Pekee kwa mafukara, na daima alifanya bidii ya kutafuta wokovu wa wakosefu (wadhambi).

Misa nzuri iliyoadhimishwa na Padre Pio ilitumia muda mrefu kwasababu ya ukimya mrefu na tafakari ya kina. Alipoulizwa ni kwanini anatumia muda mrefu katika Misa Takatifu tofauti na Mapadre wengine, alijibu; “Mungu mwenyewe anajua kwamba nataka kuadhimisha Misa kama Mapadre wengine lakini nashindwa”

Padre Pio alikuwa na mazoea ya kuungama kila baada ya masaa 10 au 12, na alitumia muda wake mwingi zaidi kuungamisha. Mtu aliyetenda dhambi ya mauti aliondolewa na kusamehewa dhambi kwa Sakramenti ya Kitubio kupitia Padre Pio alisema; najisikia kama vile natembea hewani au naelea.

Kama ilivyokuwa utotoni, Padre Pio pia katika, maisha yake, aliendelea kupata mateso makali sana kwasababu ya afya yake iliyoanza kumsumbua tangu akiwa na umri mdogo. Pia alipata majaribu mengi na makali toka kwa shetani. Mara kwa mara shetani aliposhindwa kumwangusha Padre Pio katika dhambi alimwadhibu Mtakatifu huyo kwa mapigo mbalimbali makali. Pio alikimbilia msaada wa Malaika wake mlinzi pamoja na kwa Yesu na Bikira Maria wakati wa mapambano.

Tarehe 20 septemba mwaka 1918, Padre Pio akiwa amepiga magoti na kusali mbele ya Yesu msulibiwa, kama ilivyokuwa kwa somo wake Mt. Fransisko wa Assizi, Pio alipokea alama za Madonda Matakatifu toka kwa Msulibiwa. Madonda hayo yalidumu kwa muda wa miaka 50 hadi alipofariki dunia.

Daktari aliyemchunguza Pd. Pio alisema; “hakuna sababu yoyote ya asili iliyosababisha vidonda hivyo”. Vidonda hivyo havikuathiriwa na kitu chochote na wala havikupona, bali vilinukia kama mawaridi na kuvuja damu mpaka kifo chake. Pd. Pio

No comments

Post a Comment

Shajara Yetu © all rights reserved
MKATOIKI KIGANJANI by mitume technologies