Mwezi huu wa Nane ni mwezi wa Mt. MONICA hivyo kama una hitaji kuomba juu ya ndoa yako Msogelee MUNGU kupitia maombezi ya Mt. MONICA
Tunaungana nawe kukuombea wewe mwenye uchungu mzito utokanao na maumivu katika ndoa yako
Mwezi huu tutaomba pamoja na wewe ambaye moyo wako umeinama chini kwa sababu ya makwazo mbalimbali
Tutaomba nawe wewe ambaye huyo mwenza wako kun wakati anakuweka njiapanda juu ya mambo fulani
Tutakuombea wewe mama ambaye umebebeshwa roho ya kukataliwa na upande mmoja wa ndugu wa mwanandoa wako ili Mungu akaachilia kibali cha kukubaliwa yote haya yatawezekana kwa msaada wa Muombezi wa ndoa na Mahusiano Mt. MONICA
Pia tutasema na Mungu kwa kumwinamia na kumnyenyekea aachilia uzao kwa watu wake ambao wamebeba aibu ya miaka mingi kwa kutopata watoto
Kama ndoa yako imebeba sehemu kubwa ya malalamishi yaani kila ukifanya hili hata kama ni Zurich bado tu unabebeshwa lawama...hali hii huuma sana sana bila msaada wa Mungu hakika hatuwezi songa mbele
Kwanini uendelee kuwalilia wanadamu wenzako kwa sababu ya mahusiano ama ndoa? Hamishia machozi yako kwa Bwana kwa kumwambia inatosha Bwana
Tunawaombea pia Akina mama wore Wajawazito Mungu aendelee kuwa nyumba salama ya kuishi watoto walioko matumboni mwenu
Mimba zote zenye kuambatana na changamoto yeyote ..Mungu akaachilie uponyaji na furaha wakati wa kuwaleo hawa watoto wakiwa matumboni
Tunaomba pia maombi haya yakaambatane na kuwatoa hofu akina Mama wote wajawazito kwa kuamini kwamba Mungu atawasimamia salama mpaka siku ya kujifungua
Tutaziombea pia ndoa zote zenye changamoto mbali ili zikastawi upya
Vikwazo vyote ambavyo huwa vinajiyokeza wakati ikianza mikakati ya kuzibariki ndoa ambazo hazijabarikiwa zikaweze kufunguka
Kwa imani Mungu ataenda kusimama na wewe Mama/Baba unayejiona umedhurumiwa haki yako ya upendo
Mungu akewe sababu ya kuanza upendo mpya kwenye ndoa ama mahusiano yako mpendwa
Kwa imani mwezi huu wa Agosti utakuwa ni mwezi wa kipekee kwa kuachilia msamaha wa kweli kabisa
Mungu wa Mbinguni akaipokee sala yako mbele za ifalme wake na kukuweka katika viwango vya juu zaidi
*Zaburi 141:2*
Sala yangu ipae mbele zako kama uvumba, Kuinuliwa mikono yangu kama dhabihu ya jioni.
MTAKATIFU MONICA NA WATAKATIFU WOTE WA MUNGU MTUOMBEE
No comments
Post a Comment