MAKLERO NA WATAWA NI WATU GANI?

 

Maklero ni wakina nani?
Maklero ni watu wote wenye daraja Takatifu yaani Maaskofu, Mapadri na Mashemasi.

Watawa ni akina nani?
Watawa ni Waamini, Walei au Maklero waliowekwa wakfu kwa Mungu katika Kanisa kwa ajilli ya wokovu wao na wa dunia:-
1. Kwa kufunga rasmi nadhiri za Kitawa mbele ya Kanisa
2. Kwa kuishi masharti ya injili, utii, ufukara na useja mtakatifu.
3. Kwa kufuata mtindo wa maisha uliokubalika na Kanisa

Walei ni wakina nani?
Walei ni wote katika Kanisa wasio na Daraja Takatifu

Ushirika wa Watakatifu ni nini?
Ushirika wa Watakatifu ni:-
1. Umoja na ushirikiano kati ya Wakristo Duniani, Watakatifu Mbinguni, na marehemu toharani.
2. Ni muungano wa Waamini wote katika Ekaristi Takatifu.

No comments

Post a Comment

Shajara Yetu © all rights reserved
MKATOIKI KIGANJANI by mitume technologies