MATENDO YA MWANGA (Alhamisi)
Tendo la kwanza;
Yesu anabatizwa Mto Jordani.
Tumwombe Mungu atujalie uaminifu kwa ahadi zetu za ubatizo.
Tendo la pili;
Yesu anageuza maji kuwa divai huko Kana.
Tumwombe Mungu atujalie kuukoleza ulimwengu kwa chachu ya enjili.
Tendo la tatu;
Yesu anatangaza Ufalme wa Mungu.
Tumwombe Mungu atujalie kupokea Ufalme wake kwa toba ya kweli.
Tendo la nne;
Yesu anageuka sura.
Tumwombe Mungu atujalie neema ya kuung’arisha ulimwengu kwa uso wa Yesu.
Tendo la tano;
Yesu anaweka Sakramenti ya Ekaristia.
Tumwombe Mungu atujalie neema ya kujitoa sadaka kwa ajili ya wengine.
No comments
Post a Comment