MATENDO YA MWANGA

 MATENDO YA MWANGA (Alhamisi)



Tendo la kwanza;
Yesu anabatizwa Mto Jordani.
Tumwombe Mungu atujalie uaminifu kwa ahadi zetu za ubatizo.


Tendo la pili;
Yesu anageuza maji kuwa divai huko Kana.
Tumwombe Mungu atujalie kuukoleza ulimwengu kwa chachu ya enjili.


Tendo la tatu;
Yesu anatangaza Ufalme wa Mungu.
Tumwombe Mungu atujalie kupokea Ufalme wake kwa toba ya kweli.


Tendo la nne;
Yesu anageuka sura.
Tumwombe Mungu atujalie neema ya kuung’arisha ulimwengu kwa uso wa Yesu.


Tendo la tano;
Yesu anaweka Sakramenti ya Ekaristia.
Tumwombe Mungu atujalie neema ya kujitoa sadaka kwa ajili ya wengine.

No comments

Post a Comment

Shajara Yetu © all rights reserved
MKATOIKI KIGANJANI by mitume technologies