Matendo Ya Rozari Takatifu


MATENDO YA FURAHA (Jumatatu na Jumamosi)


Tendo la kwanza;
Malaika Gabrieli anampasha habari Maria kuwa atakuwa Mama wa Mungu.
Tumwombe Mungu atujalie unyenyekevu.


Tendo la pili;
Maria Mtakatifu anakwenda kumtembelea Elizabeti.
Tumwombe Mungu atujalie mapendo ya jirani.



Tendo la tatu
;
Yesu anazaliwa Betlehemu.
Tumwombe Mungu atujalie moyo wa ufukara


Tendo la nne;

Yesu anatolewa hekaluni.
Tumwombe Mungu atujalie usafi wa moyo.


Tendo la tano;
Maria anamkuta Yesu hekaluni.
Tumwombe Mungu atujalie kuwatii wakubwa wetu.





MATENDO YA UCHUNGU (Jumanne na Ijumaa)


Tendo la kwanza;
Yesu anatoka jasho la damu kwa ajili yetu.
Tumwombe Mungu atujalie sikitiko la dhambi.


Tendo la pili;
Yesu anapigwa kwa mijeledi kwa ajili yetu.
Tumwombe Mungu atujalie kuacha dhambi za uchafu.


Tendo la tatu;
Yesu anatiwa miiba kichwani kwa ajili yetu.
Tumwombe Mungu atujalie kushinda kiburi.


Tendo la nne;
Yesu anachukua Msalaba kwa ajili yetu.
Tumwombe Mungu atujalie kuvumilia taabu.


Tendo la tano;
Yesu anakufa Msalabani.
Tumwombe Mungu atujalie kuwapenda Yesu na Maria.





MATENDO YA UTUKUFU (Jumatano na Jumapili)


Tendo la kwanza;
Yesu anafufuka.
Tumwombe Mungu atujalie kugeuka watakatifu.


Tendo la pili;
Yesu anapaa mbinguni.
Tumwombe Mungu atujalie kwenda mbinguni.


Tendo la tatu;
Roho Mtakatifu anawashukia Mitume.
Tumwombe Mungu atujalie bidii katika dini yetu.


Tendo la nne;
Bikira Maria anapalizwa mbinguni.
Tumwombe Mungu atujalie kufa vizuri.


Tendo la tano;
Bikira Maria anawekwa Malkia mbinguni.
Tumwombe Mungu atujalie kudumu katika njia njema.







MATENDO YA MWANGA (Alhamisi)


Tendo la kwanza;
Yesu anabatizwa Mto Jordani.
Tumwombe Mungu atujalie uaminifu kwa ahadi zetu za ubatizo.


Tendo la pili;
Yesu anageuza maji kuwa divai huko Kana.
Tumwombe Mungu atujalie kuukoleza ulimwengu kwa chachu ya enjili.


Tendo la tatu;
Yesu anatangaza Ufalme wa Mungu.
Tumwombe Mungu atujalie kupokea Ufalme wake kwa toba ya kweli.


Tendo la nne;
Yesu anageuka sura.
Tumwombe Mungu atujalie neema ya kuung’arisha ulimwengu kwa uso wa Yesu.


Tendo la tano;
Yesu anaweka Sakramenti ya Ekaristia.
Tumwombe Mungu atujalie neema ya kujitoa sadaka kwa ajili ya wengine.

No comments

Post a Comment

Shajara Yetu © all rights reserved
MKATOIKI KIGANJANI by mitume technologies