Matendo Ya Rozari Takatifu
MATENDO YA FURAHA (Jumatatu na Jumamosi)
Tendo la kwanza;
Malaika Gabrieli anampasha habari Maria kuwa atakuwa Mama wa Mungu.
Tumwombe Mungu atujalie unyenyekevu.
Tendo la pili;
Maria Mtakatifu anakwenda kumtembelea Elizabeti.
Tumwombe Mungu atujalie mapendo ya jirani.
Tendo la tatu;
Yesu anazaliwa Betlehemu.
Tumwombe Mungu atujalie moyo wa ufukara
Tendo la nne;
Yesu anatolewa hekaluni.
Tumwombe Mungu atujalie usafi wa moyo.
Tendo la tano;
Maria anamkuta Yesu hekaluni.
Tumwombe Mungu atujalie kuwatii wakubwa wetu.
MATENDO YA UCHUNGU (Jumanne na Ijumaa)
Tendo la kwanza;
Yesu anatoka jasho la damu kwa ajili yetu.
Tumwombe Mungu atujalie sikitiko la dhambi.
Tendo la pili;
Yesu anapigwa kwa mijeledi kwa ajili yetu.
Tumwombe Mungu atujalie kuacha dhambi za uchafu.
Tendo la tatu;
Yesu anatiwa miiba kichwani kwa ajili yetu.
Tumwombe Mungu atujalie kushinda kiburi.
Tendo la nne;
Yesu anachukua Msalaba kwa ajili yetu.
Tumwombe Mungu atujalie kuvumilia taabu.
Tendo la tano;
Yesu anakufa Msalabani.
Tumwombe Mungu atujalie kuwapenda Yesu na Maria.
MATENDO YA UTUKUFU (Jumatano na Jumapili)
Tendo la kwanza;
Yesu anafufuka.
Tumwombe Mungu atujalie kugeuka watakatifu.
Tendo la pili;
Yesu anapaa mbinguni.
Tumwombe Mungu atujalie kwenda mbinguni.
Tendo la tatu;
Roho Mtakatifu anawashukia Mitume.
Tumwombe Mungu atujalie bidii katika dini yetu.
Tendo la nne;
Bikira Maria anapalizwa mbinguni.
Tumwombe Mungu atujalie kufa vizuri.
Tendo la tano;
Bikira Maria anawekwa Malkia mbinguni.
Tumwombe Mungu atujalie kudumu katika njia njema.
MATENDO YA MWANGA (Alhamisi)
Tendo la kwanza;
Yesu anabatizwa Mto Jordani.
Tumwombe Mungu atujalie uaminifu kwa ahadi zetu za ubatizo.
Tendo la pili;
Yesu anageuza maji kuwa divai huko Kana.
Tumwombe Mungu atujalie kuukoleza ulimwengu kwa chachu ya enjili.
Tendo la tatu;
Yesu anatangaza Ufalme wa Mungu.
Tumwombe Mungu atujalie kupokea Ufalme wake kwa toba ya kweli.
Tendo la nne;
Yesu anageuka sura.
Tumwombe Mungu atujalie neema ya kuung’arisha ulimwengu kwa uso wa Yesu.
Tendo la tano;
Yesu anaweka Sakramenti ya Ekaristia.
Tumwombe Mungu atujalie neema ya kujitoa sadaka kwa ajili ya wengine.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments
Post a Comment