MASOMO YA MISA SEPTEMBER 28,2023

MASOMO YA MISA 28/09/2023
















SOMO 1
Hag 1:1-8
Katika mwaka wa pili wa Dario mfalme, mwezi wa sita, siku ya kwanza ya mwezi, neno la Bwana lilimjia Zerubabeli, mwana wa Shealtieli, liwali wa Yuda na Yoshua, mwana wa Yeosadaki, kuhani mkuu, kwa kinywa chake Hagai nabii, kusema, Bwana wa majeshi asema hivi, ya kwamba, watu hawa husema, hu sio wakati utupasao kuja, huu sio wakati wa kujengwa nyumba ya Bwana. Ndipo neno la Bwana lilikuja kwa kinywa cha nabii Hagai, kusema, Je! Huu ndio wakati wa ninyi kukaa katika nyumba zenye mapambo ya mbao, iwapo nyumba hii inakaa hali ya kuharibika? Basi sasa. Bwana wa majeshi asema hivi, Zitafakarini njia zenu. Mmepanda mbegu nyingi mkavuna kidogo; mnakula lakini hamshibi; mnakunywa lakini hamkujazwa na vinywaji; mnajivika nguo lakini hapana aonaye moto; nay eye apataye mshahara apata mshahara ili kuutia katika mfuko uliotoboka. Bwana wa majeshi asema hivi, Zitafakarini njia zenu. Pandeni milimani, mkalete miti, mkaijenge nyumba; nami nitaifurahia, nami nitatukuzwa, asema Bwana.

Wimbo wa Katikati

Zab 149:1-6, 9

Aleluya,

Mwimbieni Bwana wimbo mpya,

Sifa zake katika kusanyiko la watauwa!

Israeli na amfurahie Yeye aliyemfanya,

Wana wa Sayuni na wamshangilie mfalme wao!

(K) Bwana awaridhia watu wake.

Na walisifu jina lake kwa kucheza,
Kwa matari na kinubi wamwimbie!
Kwa kuwa Bwana awaridhia watu wake,
Huwapamba wenye upole kwa wokovu.

(K) Bwana awaridhia watu wake.

Watauwa na waushangilie utukufu,
Waimbe kwa sauti kuu vitandani mwao.
Sifa kuu za Mungu na ziwe vinywani mwao,
Na upanga mkali kuwili mikononi mwao.

(K) Bwana awaridhia watu wake.

Kuwafanyia hukumu iliyoandikwa:
Hiyo ndiyo heshima ya watauwa wake wote.

(K) Bwana awaridhia watu wake.

Shangilio
Zab 27:11
Aleluya, aleluya,
Ee Bwana, unifundishe njia yako, na kuniongoza katika njia iliyonyoka.
Aleluya.

INJILI

Lk 9:7–9
Herode mfalme alisikia habari za yote yaliyotendeka, akafadhaika kwa sababu watu wengine walisema ya kwamba Yohane amefufuka katika wafu, na wengine ya kwamba Eliya ametokea, na wengine ya kwamba mmojawapo wa manabii wa kale amefufuka. Lakini Herode akasema, Yohane nilimkata kichwa; basi ni nani huyu ambaye ninasikia mambo haya juu yake? Akataka kumwona.

No comments

Post a Comment

Shajara Yetu © all rights reserved
MKATOIKI KIGANJANI by mitume technologies